Friday, May 20, 2011

UJENZI WA SOKO YA KIJIJI CHA MBAE KATA YA UFOKONI ULIYOGHARIMU SHS 8,000,000/=

HALI YA AWALI LA SOKO LA KIJIJI CHA MBAE KABLA YA KUBOMOLEWA AN KUJENGWA UPYA NA MH HASNAIN MURJI
       HALI YA SOKO LA KIJIJI CHA MBAE HIVI SASA BAADA YA UJENZI KUKAMILIKA

 MWENYEKITI WA SOKO HILO MZEE DADI AKIFURAHIA BAADA YA SOKO KUKAMILIKA
  WAFANYABIASHARA WADOGO WA SOKO HILO WAFURAHIA SOKO JIPYA
WAFANYABIASHARA WAFURAHIA BAADA YA AHADI YA MBUNGE KUTEKELEZWA

    SOKO LA KIJIJI CHA MBAE
Wakazi wa kijiji cha Mbae walimuomba Mheshimiwa Mbunge wa Manispaa ya Mtwara – Mikindani kuwajengea soko bora la kijiji.  Hii imetokana na ubovu wa soko lao ambalo halikidhi hali bora ya soko, na limekuwa linavuja mvua ikinyesha kutokana na kuezekwa kwa makuti na kujengwa kwa miti kiasi cha kuhatarisha usalama wa wafanya biashara, afya na ubora wa bidhaa zao.
Jamii ya Mbae wamesifu na kushukuru sana utekelezaji wa ahadi alizozitoa Mheshimiwa Murji kwao.  Misaada inayoelekezwa kwao ina lengo la kuimarisha huduma za kijamii na kiuchumi.
Shukrani za dhati toka kwa wakazi wa Mbae:
Wakazi wa Mbae wameweza kutoa shukrani zao za dhati kwa Mbunge wao Mheshimiwa Murji kwa kutimiza kwa vitendo ahadi zake za kusaidia shughuli za kijamii ambazo zinaleta maendeleo kwao.                                            

No comments:

Post a Comment