Friday, May 20, 2011

UKARABATI WA HALI YA JUU MSKITI WA MBAE KATA YA UFUKONI UMEGHARIMU SH 10,000,000


1.      UKARABATI WA MSIKITI WA KIJIJI CHA MBAE
Katika kuhudumia jamii na wanainchi kwa ujumla, Mheshimiwa Mbunge wa Manispaa ya Mtwara – Mikindani ameweza kusikiliza na kutoa huduma za kijamii katika kipindi kifupi sana toka wanainchi hao wamchague kwa kura nyingi za kishindo.  Miongoni mwa shughuli za kijamii alizoanza kuzitekeleza Mheshimiwa Murji ni pamoja na kukarabati msikiti wa kijiji cha Mbae utakaowawezesha wakazi wa kijiji hicho kuwa na msikiti mzuri na wa kisasa katika kuendesha vema ibada kulingana na imani yao ya dini ya Kiislamu. Ukarabati na umaliziaji wa ujenzi msikiti wa kijiji cha Mbae umefanyika kwa kiwango kikubwa.  Ukarabati huo umehusisha msikiti wenyewe, madrasa na vyoo.                               Viongozi na waumini wafuatao waliweza kutoa shukrani zao za dhati kwa Mheshimiwa Mbunge:
·         Mr. Dadi Hamisi – Mwenyekiti wa msikiti
·         Shafii Ally Mmedi – Imamu Mkuu
·         Shaibu Dadi Hassan – Imamu Msaidizi
·         Mr. Salum Abdallah Lingondo – Mzee wa msikiti
·         Mr. Ahmad Ahmad – Mzee wa msikiti
·         Ismail Ahmad Ponda – Muumini
·         Mohamed Salum Lingondo – Muumini
·         Hassani Silim Mtondo – Muumini
·         Mr Mtiko – Msimamizi wa ujenzi na ukarabati wa msikiti.

Katika kudhibitisha ukarabati huo, wakazi na waumini wa Msikiti huo wa Mbae walishukuru kwa hatua mzuri ya ukarabati wa msikiti huo.  Pia walimshukuru Mbunge wa Manispaa ya Mtwara – Mikindani Mheshimiwa Murji kwa kutimiza ahadi alizoahidi wakazi wa kijiji hicho. 
GHARAMA ZILIZOTUMIKA KATIKA UJENZI NA UKARABARI WA MSIKITI
Jumla ya Tsh10,000,000/=. zimetumika katika ukarabati wa msikiti huo ambao umehusisha msikiti wenyewe, madrasa na vyoo.

1 comment:

  1. hongera kwa yote ila usije ukapumzika bado wana mtwara wana matatizo mengi ambayo yanataka ufumbuzi lakini nakutakia mafanikio mema katika shughuli yako ya ubunge ni mimi mwana mtwara.

    ReplyDelete