Saturday, May 21, 2011

KUSAIDIA USAFIRI KWA WANFUNZI WA SHULE MANISPAA YA MTWARA-MIKINDANI

Hali ya usafiri kwa wanafunzi wa Manispaa ya Mtwara – Mikindani hasa wale wanaosoma katika shule zilizoko pembezoni mwa Manispaa ilikuwa ni ngumu sana kutokana na kutokuwa na usafiri wa uhakika, hali iliyokuwa inawafanya wanafunzi hao kupanda malori ya mchanga ili kufikia shule zao au kurudi nyumbani.  Hali hii ilichangia kwa kiasi fulani kushuka kwa kiwango cha elimu kwa wanafunzi hao na kupelekea kuwa na matokeo mabaya katika mitihani yao.
Msaada:
Katika kukabiliana na hilo, Mheshimiwa Mbunge ameweza kutoa mabasi mawili ya wanafunzi ili kuwa na usafiri wa uhakika wa kuwahudumia wanafunzi hawa.  Hali hii imeboresha kwa kiasi kikubwa hali ya usafiri wa wanafunzi wanaosoma katika shule za sekondari za Naliendele, Mangamba na Mikindani.

No comments:

Post a Comment